Lowassa alikuwa Maziri Mkuu kati ya mwaka 2005 na 2008 kabla
ya kujiuzuLu wadhifa huo kufuatia sakata la kashfa ya rushwa iliyohusisha
kampuni ya kuzalisha umeme ya ki-Marekani Richmond Development Company LLC ya
Houston Texas.
Hata hivyo wakati anatangaza kuhamia kwake Chadema, Lowassa
alikanusha katu katu kuhusika kwa namna yoyote na kashfa hiyo na kudai kuwa
yeye alifuata tu amri kutoka kwa ‘wakubwa’ walio juu yake.
“Kama kuna mtu yeyote mwenye ushahidi basi na aende mahakamani
ama sivyo anyamaze” alisema Lowassa
“Kama kuna mtu yeyote mwenye ushahidi basi na aende
mahakamani ama sivyo anyamaze” alisema Lowassa
Kuhama kwake kunamfanya Lowassa kuwa ndie kiongozi wa kwanza
wa ngazi ya juu kabisa wa CCM kukihama chama hicho tangu kuanza kwa mfumo wa
vyama vingi nchini Tanzania mnamo mwaka 1992.
Mwanajeshi wa zamani na aliyewahi kupigana wa vita kati ya
Uganda na Tanzania mwaka 1978/79, Lowassa aliiambia hadhara kwamba akiwa kama
mtu mwenye uchungu na nchi yake isingekuwa rahisi kubaki ndani ya CCM huku
akiona chama hicho kimepoteza mwelekeo na sifa ya kuongoza nchi.
Lowassa amekimbilia upinzani baada jina lake kukatwa wakati
alipoomba kuwa mgombea urais kupitia chama tawala CCM katika uchaguzi mkuu ujao
utakafanyika mwezi Oktoba mwaka huu.
Wakati mchakato wa CCM wa kumtafuta mgombea wao wa urais
ulipoanza, Lowassa ndiye aliyekuwa kinara wa wagombea wote 42. Kila kona
aliyozunguka, mikutano yake ya hadhara ilivutia maelfu ya watu waliomuunga
mkono.
Wakati chama cha CCM kilimtaka kila mgombea apate sahihi za
wadhamini 450 lakini Lowassa alipata sahihi za wadhamini zaidi ya 700,000.
Wasifu wa Edward Lowassa
Hata hivyo mchujo wa chama ulipofanyika jina lake lilikatwa
mapema kabla hata ya kupelekwa kwenye vikao vya vya juu vya chama hicho. Ambapo
baadae Waziri wa Ujenzi John Pombe Magufuli ndiye aliyeibuka kidedea na kuwa
mgombea kupitia chama tawala CCM.
Lowassa ameushutumu mchakato CCM wa kutafuta mgombea urais
akiuita kuwa ulijaa chuki na mizengwe dhidi yake, hali ambayo aliifananisha na
‘ubakaji wa demokrasia’
“Nitakuwa mnafki nikisema bado nina imani na CCM. CCM
niliyoiona Dodoma si CCM niliyokulia”, alisema, na kuongeza “kama Watanzania
hawapati maendeleo kupitia CCM basi wakayatafute nje ya CCM”
Wakati sakala la Richmond lilipoibuka miaka michache tu
iliyopita, Chadema ilimfanya limsakama Lowassa kuwa ni mmoja wa mafisadi
wakubwa nchini. Lakini wakati chama hicho kinamkaribisha kuwa mwanachama wao,
kiligeuka na kusema hakuna mtu msafi nchini na kwamba hawawezi kuacha kumpokea
mwanasiasa mwenye mtaji mkubwa wa wafuasi kama Lowassa.
Wakati akiwa Waziri Mkuu, Lowassa alisifika kama mchapakazi
hodari na msimamiaji wa moja kwa moja wa shughuli za serikali. Bado anaendelea
kufahamika kwa jina la utani la ‘mzee wa maamuzi magumu’.
Je unamfahamu Edward Lowassa ni nani katika siasa za
Tanzania ?
Moja ya mafanikio makubwa ya uwaziri mkuu wake ni jitihada
kubwa na mafanikio ya upatikanaji wa fedha za kujenga chuo kikuu cha Dodoma.
Chuo hiki kikuu cha umma kilichopo katikati ya Tanzania kilianzishwa mwaka
2007.
Lowassa ni mashuhuri pia kwa kusimamia mpango wa serikali
uliofanikiwa wa ujenzi wa shule za kata ambazo uliiletea Tanzania sifa kubwa
kwa kutoa fursa ya watoto wengi kupata nafasi shuleni.
Mtoto wa Mzee Ngoyai Lowassa, ambaye aliwahi kuwa mtumishi
wa serikali ya kikoloni, Lowassa ameanza harakati zake za kuwania urais tangu
mwaka 1995 lakini inaarifiwa kwamba rais wa kwanza wa Tanzania Mwl Julius
Nyerere alimkatalia kushika nafasi hiyo. Wafuasi wa Lowassa wamekuwa
wakiyatupilia mbali madai hayo
Ulipofika uchaguzi wa mwaka 2005, Lowassa hakutaka kuwania
urais, lakini badala yake alimnadi rafiki yake wa siku nyingi Rais wa sasa
Jakaya Kikwete ambaye alipata ushindi wa kishindo wa zaidi ya asilimia 80.
No comments:
Post a Comment