Ibada maalumu za ukumbusho zinaendelea kufanywa katika mji
wa Nagasaki, nchini Japan, kuadhimisha miaka 70 tangu kulipuliwa kwa bomu ya
atomiki jijini humo.
Katika ibada hiyo mzee mmoja aliyenusurika aliibua hisia
baada ya kukashifu hatua ya serikali iliyokomadarakani kwa kubadili vipengee
vya katiba ya nchi hiyo ilikuruhusu wanajeshi wake kushiriki katika vita.
Manusura wa bomu hiyo ya Nyuklia iliyoua zaidi ya watu laki
mbili
Maelfu ya watu waliohudhuria ibaada hiyo ya ukumbusho
walimpigia makofi kwa uwazi wake.
Meya wa mji wa Nagasaki naye alivutia waya huohuo
akimkashifu waziri mkuu bwana Shinzo Abe kwa jitihada za kubadilisha katiba ya
nchi.
Wazungumzaji wamekashifu hatua ya serikali iliyokomadarakani
kwa kubadili vipengee vya katiba ya nchi hiyo ilikuruhusu wanajeshi wake
kushiriki katika vita.
Bwana Abe alikaa kimya kando tu jukwaani.
Bomu hilo lilidondoshwa na wanahewa wa Marekani, siku tatu
tu baada ya kudondosha lingine la kinukilia katika jiji la Hiroshima.
Bomu hilo lilidondoshwa na wanahewa wa Marekani, siku tatu
tu baada ya kudondosha lingine la kinukilia katika jiji la Hiroshima.
Bomu hilo liliangamiza kabisa mji huo na kuua watu zaidi ya
70,000 .
Inakisiwa kuwa zaidi ya watu 200,000 waliuawa katika
milipuko hiyo miwili, na wengine kufariki baadaye kutokana na miale ya sumu
kutoka kwa mabomu hayo ya nguvu za kitonaradi.
|
No comments:
Post a Comment